TANZANIA MIONGONI MWA NCHI 5 UTEKELEZAJI WA KUKABILIANA NA DHARURA NA MAJANGA AFRIKA

Na. Catherine Sungura, Wizara ya Afya-Dodoma Tanzania ni miongoni mwa nchi 5 kati ya 17 za awamu ya kwanza barani Afrika  zitakazotekeleza mradi wa kuwajengea uwezo wa sekta ya afya kujiandaa, kugundua na kukabiliana na dharura na majanga. Wataalamu wa sekta ya mbalimbali wanaoshirikiana na sekta ya afya katika  kukabiliana na dharura na majanga wameshiriki.